Psalms 22:1-3

Kilio Cha Uchungu Na Wimbo Wa Sifa

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Utenzi Wa Kulungu Wa Alfajiri. Zaburi ya Daudi)


1 aMungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?
Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa?
Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?

2 bEe Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu,
hata usiku, sinyamazi.


3 cHata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu;
wewe ni sifa ya Israeli.
Tafsiri zingine zinasema: uketiye juu ya sifa za Israeli.

Copyright information for SwhKC